Wema Isaac Sepetu ‘akidendeka’ chumbani na mwanaume.
Kipande cha video kilichosambaa kwenye Mitandao ya Kijamii ya Instagram, Facebook na WhatsApp kikimuonesha staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘akidendeka’ chumbani na mwanaume kimemuweka pabaya baada ya Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Joyce Fisoo kusema kuwa kama ni sehemu ya filamu haina maadili ya Kitanzania.
Kipande hicho cha filamu hiyo kinamuonesha Wema akiwa anadendeka kikwelikweli na jamaa huyo jambo ambalo bodi hiyo imeliangalia kwa upande wa pili na kwamba haitaingia sokoni ikiwa hivyo.
“Jamani hata kama ni filamu, hapana, imezidi, kwa kweli ni hatari sana maana kama Wema angekuwa mwanamke wangu hata hiyo filamu angeacha kuicheza kabisa,” alisema mmoja wa mashabiki hao.
“Yaani na mimi napenda sana nicheze filamu vipande kama hivyo ishirini hivi tena nitacheza vizuri sana maana najua kila mtu anaweza kuigiza kama hivyo,” alisema Idris.
Kwa upande wake Wema hakutaka kusema chochote juu ya kipande hicho.
Tupe Maoni Yako Kuhusu Habari Hii