Showing posts with label AFYA. Show all posts
Showing posts with label AFYA. Show all posts

Tuesday, October 25, 2016

Vyakula Vinavyoongeza Hamu na Nguvu ya Kufanya Tendo la Ndoa


Tatizo la uwezo wa kufanya tendo la ndoa linazidi kukua miongoni wa wanandoa na wapenzi wengi. Takwimu za kitafiti zinaonyesha kuwa karibu ndoa 4 kati ya 10 zenye umri wa miaka 3 na kuendelea zinakabiliana na tatizo hili. Aidha wanaume 6 kati ya 10 wanatajwa kulalamikia upungufu wa nguvu za kiume.

Pamoja na matatizo mengine kutajwa kuchangia upungufu wa nguvu za kiume na kushuka kwa msisimko wa tendo miongoni mwa wanandoa, uchunguzi umeonesha kuwa utumiaji holela wa vyakula hasa vyenye mafuta ni moja kati ya sababu zinazochangia kwa kasi tatizo hili.

Kwa kuzingatia hilo, watafiti wa masuala ya uhusiano wa kimapenzi wamebaini aina mbalimbali ya vyakula ambavyo vina uwezo wa kumuongezea mtu nguvu ya kufanya tendo la ndoa.  Vyakula hivyo ni hivi vifuatavyo:

1. PILIPILI
Kama tunavyojua wote mara nyingi chakula ambacho kimeungwa pilipili hufanya hata mapigo ya moyo kuwa tofauti na wakati mwingine hata jasho au kamasi hutoka. Ndani ya pilipili kuna kitu kinaitwa capsaicin ambacho hufanya pilipili iwe na hali ya ukali. Capsaicin huwezesha ubongo kutoa homoni ya endorphins ambayo huleta mgusu wa hisia za raha wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Pia pilipili husisimua mfumo wa fahamu (nerves) wa ubongo na katika kufanya hivyo huwezesha kuamshwa haraka kimapenzi (kunyegeka) wakati wa tendo la ndoa na pia ukiguswa au kubusiwa au kunyonywa au kupapaswa unapata hisia kila sehemu ya mwili.

2. MATUNDA NA MBOGA ZA MAJANI
Ulaji wa matunda na mboga za majani una matokeo makubwa sana katika hamu ya tendo la ndoa kwa njia nyingi. Kwanza matunda na mboga za majani hupunguza kiwango cha mafuta na unene (cholesterol).  Kuongezeka kwa mafuta mwilini huzuia mzunguko wa damu kwa kubana mishipa ya damu.

Pia kula matunda na mboga za majani huhakikisha balance ya uzito kwani unene (obesity) kwa wanaume kuna matokeo mabaya katika kuzalisha homeni za testoeterone na hatimaye jogoo kushindwa kuwika na kuwa na pia mwanaume anakuwa na hisia za mapenzi (libido) kidogo.
Na pia wanandoa wanapozidi kunenepeana ndipo na hali ya kufurahia au kuwa na hamu ya tendo la ndoa huzidi kupungua. Kitalaam inashauriwa kula milo (potions) 3-5 za matunda kwa siku.

3. NAFAKA ZISIZOKOBOLEWA
Nafaka hasa zisizokobolewa kama mahindi, ngano, uwele, nk zina nyuzinyuzi (fibre) na sukari ngumu (complex sugar) ambazo kusaidia kutunza uzito wa mwili. Nafaka husaidia katika kuzalisha homoni za testosterone kwenye damu. Na pia nafaka huwezesha mtu kuwa na nguvu hatimaye kwenda masafa marefu wakati wa tendo.

Kula nafaka nzima kama vile brown bread badala ya white bread, pia kula nafaka halisi badala ya cornflakes ni jambo zuri linalokuhakikisha afya nejama na mahusiano mazuri ya ndoa yako.

4. TANGAWIZI
Tangawizi ni kiungo cha mboga ambacho husisimua sana na kusaidia mfumo wa mzunguko wa damu mwilini. Tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume hivyo kuwa na umuhimu sana katika kuboresha ufanyaji wa tendo la ndoa. Inaweza kuliwa mbichi, au kuliwa ikiwa imeungwa kwenye chakula au kusagwa na kuwa kama unga na kutumiwa kama chai.

5. ASALI
Asali ina madini yanayoitwa boron, ambayo husaidia mwili kutumia homoni ya estrogen ambayo ni homoni inayohusika na viungo ya uzazi na mapenzi kwa mwanamke.
Pia kuna utafiti unaoonesha kwamba asali huongeza nguvu, kitendo ambacho kitapelekea mwanamke kuwa uwezo na hamu ya tendo la ndoa au libido.

6. KARANGA
Karanga huhusika katika kuchochea mfumo wa mzunguko wa damu (vascular system). Mzunguko wa damu ulio sawasawa katika uke na uume huwezesha mwanaume na mwanamke kupata msisimko wa mapenzi haraka hatimaye tendo la ndoa kuwa murua. Pia karanga zina madini muhimu kama vile magnesium, asidi ya folic na zinc ambayo ni muhimu sana katika usalishaji wa mbegu za mwanaume.

7. CHAZA (OYSTERS) NA PWEZA
Hawa ni aina ya samaki ambao hupatikana katika maji chumvi. Huwa na kiasi kikubwa sana cha madini ya zinc na haya madini ndiyo huhusika zaidi na uzalishaji wa homoni ya testosterone kwa wanaume.
Pia imethibitika kwamba wanaume wenye ukosefu wa madini ya zinc huwa na matatizo ya nguvu za kiume.  Pia madini mengi ya zinc mwilini huongeza kiwango cha shahawa kwa wanaume.

8. SOYA
Pamoja na kuwa na kiwango kidogo sana cha mafuta (fat) na pia kuwa na kiwango kizuri cha protein, soya zina phytoestrogens ambayo husaidia sana wanawake ambao wamefikia menopause kutengeneza homoni estrogen ya ziada.
Husaidia uke kuwa laini (wet, lubricated) mwanamke akisisimuliwa wakati wa tendo la ndoa.

9. CHOKOLETI
Chocolate ina phenylethylamine, kemikali ambayo husababisha hisia (feelings) za furaha wakati wa mwanamke au mwanaume kufika kileleni (orgasm). Inasaidia sana kula chocolate masaa machache kabla ya kuanza kufanya tendo la ndoa.

10. PARACHICHI
Aina nyingine ya chakula ambacho husaidia kuongeza uwezo wa mtu kufanya tendo la ndoa ni Parachichi. Tunda hili linauwezo mkubwa wa kuzalisha vitamini E ambayo husaidia katika uzalishaji wa homoni. Inatajwa kuwa watu wanaotumia tunda hili kwa wingi huwana msisimko mkali wa kimapenzi na kwa upande wa wanawake husaidia kuongeza majimaji yenye utelezi sehemu za siri na hivyo kuzuia uwezekano wa kuchubuka wakati wa kujamiiana.

Sunday, October 9, 2016

CHINa Yapiga Marufuku Nyama ya Kuku


Serikali ya China yapiga marufuku uuzaji za kuku zilizozalishwa kwa mbinu mpya ya uzalishaji kwa kutumia homoni .

Raia wengi nchini China wameripotiwa kuwa na maradhi yanayosababishwa na homoni zinazopatikana katika proteini ya nyama ya kuku.

Wizara ya afya ya umma imetangaza kuwa makampuni yote ya kuuza nyama ya kuku kufungwa na viwanda vitakavyokiuka sheria hiyo mpya vitapewa adhabu kali.

Kwa sasa kuku waliozalishwa kwa kutumia hormoni na antibiyotiki wanauzwa karibu kila pande ya dunia .

Wazalishaji wa kuku hizi kwa ajili ya biashara hutumia hormoni na antibiyotiki ili kuharakisha kukomaa kwa kuku hawa .

Wednesday, October 5, 2016

Dawa ya asili ya ugonjwa wa moyo

Ugonjwa wa moyo  unajumuisha matatizo ambayo yanaathiri muundo na kazi za MOYO. Ugonjwa wa moyo mara nyingi huhusishwa na kujibana au kukazika kwa mishipa ya damu, au mkusanyiko wa taka katika kuta za mishipa ya damu ambako hupelekea kupungua kipenyo cha mishipa ya damu na hivyo kuzuia mzunguko ulio huru wa damu, na hatimaye kukupa hatari ya kupata shambulio la moyo na stroke.

Ugonjwa wa moyo unahusisha matatizo kama matatizo ya mishipa ya moyo, matatizo ya kurithi ya moyo, mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida, moyo kufeli kufanya kazi, matatizo ya valve za moyo, moyo mpana au mkubwa na matatizo mengine mengi katika moyo.

 Chanzo na dalili za ugonjwa wa moyo hutofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine kutegemea na aina ya ugonjwa wa moyo. Baadhi ya dalili za kawaida ni pamoja na pumzi fupi, maumivu ya kifua, mapigo ya chini ya moyo, kichwa kizito, uchovu na udhaifu wa mwili kwa ujumla.

Vitu vingine vinavyoweza kuongeza hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo ni pamoja na:

a)Shinikizo la juu la damu
b)Kolesto
c)Kisukari
d)Uzito kupita kiasi
e)Uvutaji sigara
f)Unywaji pombe kupita kiasi
g)Matumizi yaliyozidi ya kaffeina
h)Utumiaji wa madawa ya kulevya
i)Uzee
j)Kutokujishughulisha na mazoezi
j)Kurithi
k)Mfadhaiko wa akili (stress)

Wakati unataka kujitibu ugonjwa wa moyo ni mhimu kutofanya lolote wewe mwenyewe peke yako bila ushauri au uangalizi wa karibu wa daktari au muuguzi wako. Unaweza pia kutumia baadhi ya dawa za asili na kubadili namna unavyoishi ili kuimarisha afya ya moyo wako.

Baadhi ya hizi dawa za asili zinaweza zisipatane na baadhi ya dawa za hospitalini kama upo unatumia dozi ya ugonjwa fulani wakati huu. Kwahiyo pata ushauri kwanza toka kwa mtaalamu wa afya aliye karibu na unayemwamini kabla hujaamua kutumia baadhi ya hizi dawa.

1. Mafuta ya Habbat Soda
Moyo usio na afya unaweza kuwa ni matokeo ya sababu nyingi sana lakini chanzo kikuu cha sababu zote hizo ni kimoja, nacho ni kutokuupa moyo virutubishi mhimu unavyovihitaji kila siku ili ubaki na afya.

Mafuta ya asili ya Habbat Soda yana kiinilishe mhimu sana kwa afya ya moyo ambacho ni asidi amino Omega 6 na 9 na kiilishe kingine kijulikanacho kwa kitaalamu kama ‘phytosterols’. Viinilishe hivi mhimu husaidia kuzuia mishipa kujikaza na hivyo kuwa msaada mkubwa hata kwa ugonjwa wa shinikizo la juu la damu. Viinilishe hivi kwenye mafuta asili ya habbat soda husaidia kushusha kolesto na sukari katika damu pia.

Kwa karne nyingi mafuta ya asili ya habbat soda yamekuwa yakitumika kutibu ugonjwa moyo.
Kunywa kijiko kidogo kimoja cha chakula cha mafuta haya kutwa mara 2 kwa majuma hata miezi kadhaa. Unaweza kuchanganya mafuta haya kwenye glasi moja ya juisi yoyote uliyotengeneza nyumbani ili kuupata radha.

2. Kitunguu Swaumu
Tafiti kadhaa zimeonyesha kitunguu swaumu kuwa na ufanisi mkubwa sana katika kutibu magonjwa kama shinikizo la juu la damu, kolesteroli na magonjwa ya mishipa ya moyo. Kitunguu swaumu huzuia kujikaza au kuzibika kwa mishipa ya damu. Kitunguu swaumu pia huongeza msukumo wa damu. Ili kujitibu au kujizuia usipate ugonjwa wa moyo kwa kitunguu swaumu fanya hivi;

Kula punje moja au mbili za kitunguu swaumu kila siku. Ikiwa inakutokea radha yake au harufu yake inakuwa kali sana unaweza kunywa glasi moja ya maziwa freshi baada ya kuwa umekula hizo punje za kitunguu swaumu.
 Mhimu: Kitunguu swaumu kinaweza kisipatane na aina nyingi ya dawa za hospitalini sababu ya baadhi ya dawa hizo hukaza mishipa ya damu. Wasiliana na daktari wako kabla ya kuanza kutumia hii dawa.

3. Bizari (manjano)
Tafiti zinaonyesha kwamba bizari inao uwezo wa kuzuia mishipa ya damu kujikaza. Bizari inayo kirutubishi mhimu sana kijulikanacho kwa kitaalamu kama ‘curcumin’ ambacho husaidia kutunza afya ya moyo kwa kuzipunguza taka taka za kolesto, takataka nyingine zozote kwenye mishipa ya damu na kuzuia kuganda kwa damu kwa ujumla.

Bizari pia inasaidia kushusha msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto ((LDL) na kuzuia uundwaji wa uvimbe. Inao uwezo mkubwa pia wa kuondoa sumu mwilini na hivyo kuzuia kujijenga kwa vijidudu nyemelezi vya magonjwa (free radicals) na kama matokeo yake ya pili husaidia kutozeeka mapema na magonjwa mengine sugu.

Tumia bizari mara nyingi au kama kiungo kwenye vyakula vingi unavyopika.
Unaweza pia kuchemsha kijiko kikubwa kimoja cha chakula na maji nusu  lita au na maziwa nusu lita (vikombe viwili). Kunywa  kikombe kimoja asubuhi na kikombe kingine jioni  kila siku kwa wiki kadhaa.

4. Uwatu
Uwatu una sifa kuu ya kuondoa sumu mwilini na kuulinda mfumo mzima wa upumuaji. Uwatu husaidia kupunguza uwezekano wa ateri za damu kuzibika (atherosclerosis), hurekebisha na kuweka sawa usawa wa mafuta katika damu (blood lipid).

Uwatu pia husaidia seli damu za damu kutokuumana na kukaribiana sifa ambayo ni mhimu sana katika kuzuia damu kuganda na hivyo kupunguza hatari kugandana au kushikana kwa seli za damu kusiko kwa kawaida kunakohusiana na shambulio la moyo, kushusha kolesto, sukari katika damu na mafuta yaliyozidi.


  • Loweka kijiko kidogo kimoja (kijiko cha chai) cha mbegu za uwatu kwa usiku mzima.
  • Siku inayofuata kula hizo mbegu za uwatu zilizokuwa zimeloweka wakati tumbo likiwa tupu.
  • Fanya hivyo kila siku kwa miezi kadhaa.

5. Chai ya kijani (Green Tea)
Chai ya kijani maarufu kama ‘Green tea’ ina viondoa sumu vya mhimu sana mwilini ambavyo husaidia kuimarisha afya ya seli zinazounda sehemu ya ndani kabisa za moyo na mishipa ya damu. Husaidia kushusha kolesto na kiwango cha mafuta katika damu. Chai hii pia husaidia kudhibiti sukari katika damu (blood sugar) na kuimarisha mfumo wa mmeng’enyo wa chakula.

Katika utafiti uliofanywa na Japani mwaka 2008, watafiti waligundua kuwa kunywa vikombe vitano vya chai hii ya kijani kwa siku kulisaidia kupunguza hatari ya kupatwa na vifo vinavyotokana na ugonjwa wa moyo au stroke kwa asilimia 26.

Kunywa vikombe vinne kila siku vya chai hii ya kijani (kumbuka usiongeze ndani yake yale majani mengine meusi ya chai ili kuepuka kaffeina).

6. Mazoezi
Utanishangaa mazoezi nayo ni dawa? Ndiyo mazoezi ni dawa tena ni dawa kwa magonjwa mengi sana mwilini tofauti na unavyodhani. Tatizo watu wengi hawajishughulishi na mazoezi labda mpaka waambiwe au washauriwe na daktari. Mazoezi ni mhimu kwa mtu yeyote uwe unaumwa au huumwi chochote.

Mazoezi ya mara kwa mara yakiambatana na kula lishe sahihi inaweza kusaidia kuzuia na kuudhibiti ugonjwa wa moyo. Mazoezi kama ya kutembea  kwa miguu, kukimbia pole pole (jogging), kuendesha baiskeli  na kuruka kamba ni mazoezi ya mhimu sana katika kuuongezea nguvu moyo wako na mfumo wa upumuaji, kuimarisha mzunguko wa damu na kushusha shinikizo la juu la damu.

Mazoezi husaidia pia kudhiti uzito na unene kupita kiasi wa mwili na hivyo kupunguza msongo wa mawazo (stress) vitu ambavyo vina uhusiano wa karibu kati ya ugonjwa wa moyo na magonjwa mengine mengi.

Chama cha madaktari wa magonjwa ya moyo cha Marekani kinashauri kila mtu kufanya mazoezi ya walau nusu saa kila siku mara tano kwa wiki ili kuimarisha afya ya moyo na kupunguza hatari ya kupata ugonjwa wa moyo. Ongea na daktari juu ya mazoezi gani yanakufaa kwa mjibu wa uzito wako.

7. Magnesium na Potassium
Utafiti mmoja umeonyesha kuwa kutumia madini ya magnesium kunaweza kupunguza shinikizo la juu la damu na kwamba ni madini mazuri kwa ufanyaji kazi wa jumla wa moyo.

Utafiti mwingine umeonyesha utumiaji wa potassium unasaidia kuboresha kazi za moyo vile vile husaidia kupunguza shinikizo la juu la damu kutokana na utumiaji uliozidi wa chumvi.

Unaweza kuwa umeshaambiwa kuwa utumiaji wa chumvi ya mezani (sodium chloride) ni jambo baya, lakini kwa kutumia chumvi yenye magnesium na potassium badala ya chumvi ya mezani kunaweza kusaidia sana kushusha shinikizo la juu la damu kama inavyoelezwa kwenye utafiti huu.

Mambo ya mhimu kuzingatia:

  • Punguza mafuta, kolesto na chumvi kwenye chakula chako.
  • Epuka mafuta magumu hasa yale yatokanayo na wanyama (polyunsaturated and monounsaturated fats). Mfano unaweza kutumia mafuta ya zeituni badala ya kutumia siagi, margarine na mafuta mengine yatokanayo na wanyama.
  • Acha kuvuta sigara na punguza kunywa pombe
  • Punguza uzito, hakikisha una uzito kulingana na urefu wako.
  • Punguzo mawazo (stress) na tumia mbinu mbadala za ku-relax (kupumzika).
  • Epuka ugonjwa wa kisukari.
  • Pata vitu vyenye omega 3 na vitamin D
  • Pata usingizi wa kutosha kila siku.
  • Fanya vipimo vya jumla juu ya afya yako kila mara.

Je Umeipenda makala hii? Ninakaribisha mchango wako wa mawazo au ikiwa una swali nitafurahi zaidi kwani ni faraja kwangu kuona nimekujibu vizuri.

Thursday, September 22, 2016

FAHAMU SULUHISHO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Ukweli ni kwamba ndoa nyingi za Kikristo zinavunjika kutokana na tatizo hili. Je, hakuna haja ya kuitisha mjadala wa kitaifa? Taifa letu linaangamia kwa kukosa maarifa.

Hivi upungufu wa nguvu za kiume ni nini? Kifupi ni mwanamume kutokuwa na uwezo wa kutoa mbegu bora zenye uwezo wa kutungisha mimba, au kutosimama kwa uume.

Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa asilimia 60 ya wanandoa nchini wanakabiliwa tatizo hili. Kwa hiyo, mabango ya waganga yaliyopo barabarani hayajapunguza kabisa tatizo hilo.

Hawa watu wanatibu watu au majini? Hapo ndipo kiini cha makala haya. Sababu kubwa ya ongezeko la wenye matatizo haya ni kwamba dawa nyingi zinazodaiwa kuponya tatizo hili hazina viwango vya kuitwa dawa, bali ni vichocheo tu kwani kinachopigiwa chapuo huwa ni kumudu tendo kitandani na si nguvu asilia.

Waganga wengi wameelekeza nguvu zao huko na ni hapo ndipo janga hili la kitaifa linapoota mizizi.

Ukweli ni kwamba upungufu wa nguvu za kiume hauondolewi kwa dawa za kuchochea nguvu wakati wa tendo. Hizi zina madhara makubwa na mara kadhaa husababisha vifo kwa wanamume wengi wakiwa ‘guest’ na vimada wao kwani hulipua moyo.

Ni lazima kiini cha tatizo hili kichunguzwe na tiba stahiki ipatikane. Kinyume cha hapo, janga hili linaweza kugeuka na kuwa dubwana kubwa la kutumaliza.

Matatizo ya nguvu za kiume huchangiwa na kuugua kwa muda mrefu, ugonjwa wa kisukari, kuvaa nguo za kubana sana, mionzi ya simu, kompyuta na mengineyo. Pia dawa za kuua wadudu huleta tatizo hili kwani zina viambata sumu viitwavyo ‘estrogen’, matatizo ya kisaikolojia, kupiga punyeto kwa muda mrefu na kutumia vyakula vyenye kemikali.

Utafiti unasema kuna uhusiano mkubwa sana kati ya upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na sumu mwilini zinazotokana na vyakula vyenye kemikali tunavyobugia kwa kupenda au kutokupenda.

Ni kutokana na utafiti huo ndipo dawa bora yenye uwezo mkubwa wa kuondoa sumu mwilini kwa muda mfupi ikagunduliwa. Hii ikiwekwa kwenye kinywaji chochote chenye kemikali, mara moja hutenganisha sumu iliyomo humo.

Dawa hii pia huleta nguvu za kudumu za kiume, hujenga afya na kuleta nguvu asilia. Hutatua tatizo la nguvu za kiume huku ukiondoa pia tatizo la ugumba na ni vizuri wenye matatizo kama hayo wakatumia vyakula vya protini hasa ya mimea kwani hurutubisha mbegu.

Kuna aina 2 ya vyakula ambavyo vimefanyiwa utafiti na kubaini kuwa ni moja ya vyakula vinavyosaidia kuongeza nguvu za kiume na havina madhara katika engezeko la nguvu za kiume, katika vyakula hivyo vyenye uwezo wa kuongeza nguvu za kiume kiasili ni:

1. TANGAWIZI
- Tangawizi ni moja ya chakula kinachoweza kurejesha nguvu za kiume, unaweza kuichemsha tangawizi na ukatumia kwa kuinywa kama chai Asubuhi, mchana na jioni pia Tangawizi unaweza ukaitumia katika mchanganyiko wa kiasili kwa kutumia habat soda,asali,kitunguu saumu na tangawizi yenyewe. JINSI YA KUTUMIA MCHANGANYIKO HUU: Chukua tangawizi na kitunguu saumu vitwange kisha vichanganye na asali pamoja na unga wa habat soda na uwe unakunywa mchanganyiko huu kwa kutumia kijiko cha chai kimoja kutwa mara 3 kwa muda wa wiki moja na utaona mabadiliko.

2. TIKITI MAJI:
-Chakula kingine kinachosaidia katika upande wa kuongeza nguvu za kiume ni tunda la Tikiti Maji, unaweza ukachukua tikiti lako ukalikata na kutengeneza juice ya Tikiti kisha unakunywa ila sio lazima utengeneze Juice hata lenyewe tu unaweza ukalila. Ila jitahidi kutumia tunda hili hata kila siku kwani linasaidia sana kwa wenye matatizo ya nguvu za kiume.

Sunday, September 4, 2016

Faida 48 za Juisi ya Tangawizi ambazo ulikuwa huzijuwi bado

FAIDA 48 ZA JUISI YA TANGAWIZI AMBAZO ULIKUWA HUZIJUWI BADO
13906892_639674622864710_3940101601465448113_n
Huwa inanishangaza sana ninapoutafakari ukuu wa Mungu kwa namna ambayo ametupa mimea mbalimbali mhimu kwa ajili ya afya zetu – Mwanzo 1:29. Maelezo yafuatayo kuhusu tangawizi yatakupa wewe ujuzi wa mmea mwingine wa asili usio na madhara ya kikemikali na kusaidia mwili wako kuwa na afya nzuri na ya kupendeza.
Tafiti mpya zinazidi kuonyesha namna mmea huu ulivyo wa mhimu kwa afya ya binadamu ikihusisha uwezo wake wa kudili na aina mbalimbali za kansa mwilini na tafiti nyingine zinaendelea kufanyika.
Tangawizi inaweza kuwekwa karibu kwenye kila chakula, iwe ni katika kuilainisha nyama nyekundu, kuongeza radha katika nyama au samaki, kama chai, kwenye juisi na kadharika. Binafsi napenda ikiwa kwenye juisi ya matunda ndiyo inakuwa tamu zaidi na inaenda kufanya kazi mwilini haraka zaidi.
Tangawizi ni zao la kibiashara na ni rahisi kutoka kimaisha kama utaamua kulima tangawizi ingawa ni zao la miezi mingi lakini ukivumilia utakula bata tu, gunia moja linauzwa kati ya laki 3 hadi 6 wakati wa msimu mzuri.
Tangawizi iliorodheshwa kwa mara ya kwanza na serikali ya Marekani kama dawa kwa ajili ya binadamu kati ya mwaka 1820 na 1873.
Tangawizi huongezwa pia katika vinywaji vingi vya viwandani zikiwemosoda ili kupata radha nzuri zaidi.
Leo nimekuletea hii juisi ya tangawizi, nimetumia tangawizi mbichi za ukubwa wa kati nne, parachichi moja na asali mbichi vijiko vikubwa saba na na maji lita moja na nusu.
Kazi 48 za tangawizi mwilini
1. Huondoa sumu mwilini haraka sana
2. Huua bakteria wa aina nyingi mwilini hata salmonella ndani ya mwili hata juu ya ngozi
3. Kuna viua vijasumu (antibiotics) vya asili viwili kwenye tangawizi
4. Huondoa uvimbe mwilini
5. Huondoa msongamano mapafuni
6. Tangawizi inayo ‘zingibain’ ambayo huua vimelea mbalimbali vya magonjwa na mayai yake
7. Huondoa maumivu ya koo
8. Huua virusi wa homa
10. Huondoa homa hata homa ya baridi (chills)
11. Hutibu saratani ya tezi dume. Tangawizi huua kimeng’enya ambacho ni chakula cha seli za kansa ya tezi dume kiitwacho ‘5-LO enzymes’ na seli hizo za kansa hufa ndani ya masaa mawili au manne bila hicho kimeng’enya.
12. Tangawizi ina kiinilishe mhimu sana ambacho huzuia kuongezeka kwa seli za kansa ya kongosho kiitwacho kwa kitaalamu kama ‘gingerol”
13. Hutibu kansa zinazoweza kusababishwa na kupata choo kigumu muda mrefu (constipation-related cancer)
14. Ni dawa nzuri kwa kansa ya kwenye damu (leukemia)
15. Ni dawa nzuri dhidi ya kansa ya mapafu (lung cancer)
16. Huzuia kujizalisha kwa bakteria aitwaye ‘Helicobacter pylori’, bakteria huyu ndiye husababisha vidonda vya tumbo mwilini, pia hutibu kiungulia, na kanza mbalimbali za tumbo
17. Ni msaada sana katika kuzuia na kutibu kansa ya titi
18. Hutibu kanza za kwenye kizazi na kanza za kwenye mirija ya uzazi
19. Huongeza msukumo wa damu
20. Husaidia kuzuia shambulio la moyo
21. Huzuia damu kuganda
22. Hushusha kolesto
23. Husafisha damu
24. Husaidia watu wenye kukakamaa kwa mishipa
25. Hutibu shinikizo la juu la damu
26. Husafisha utumbo mpana
27. Hupunguza mishtuko kwenye utumbo mpana na tumbo kuunguruma
28. Huondoa GESI TUMBONI KIRAHISI ZAIDI
29. Husaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula
30. Dawa nzuri ya kuondoa uchovu
31. Husaidia kuzuia kutapika. Husaidia hata wale wanaosafiri baharini wasipatwe na kichefuchefu
32. Husaidia kuondoa maumivu kutokana na mkao mmoja wa mrefu ama kusimama au kukaa
33. Husaidia uzalishwaji wa juisi vimeng’enya kwa ajili ya kumeng’enya chakula
34. Husaidia kuzuia kuharisha
35. Husaidia mfumo wa upumuaji na kutuliza dalili za pumu
36. Hutibu tatizo la miguu kuwaka moto
37. Hutibu homa ya kichwa
38. Hutibu maumivu ya tumbo wakati wa hedhi
39. Hutibu homa za asubuhi hata kwa mama mjamzito
40. Husaidia kupunguza homa ya baridi yabisi (helps reduce inflammation of arthritis)
41. Huimarisha afya ya figo
42. Husaidia kupunguza uchovu unaotokana na matibabu yaliyopita ya mionzi
43. Ina madini ya potassium ya kutosha
44. Ina madini ya manganese ambayo ni mhimu katika kuuongeza mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali, hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita
45. Ina kitu kinaitwa ‘silicon’ ambacho chenyewe kazi yake hasa ni kuongeza afya ya ngozi, nywele, meno na kucha
46. Husaidia umeng’enywaji wa madini ya calcium
47. Pia ina vitamini A, C, E, B-complex, chuma, zinki , magnesium, phosphorus, sodium, calcium, na beta-carotene
48. Hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita
 

GOSSIPS Copyright © 2016 -- Template created by Mbatta