Thursday, May 26, 2016

Davina alia filamu za mapenzi kuua soko

davinaNa Gladness Mallya
Muigiza wa long time Bongo, Halima Yahya ‘Davina’ ameibuka na kueleza kwamba filamu za mapenzi wanazocheza wasanii wengi zimeua soko ndiyo maana kwa sasa ni kama sanaa hiyo haipo.
Akichonga na paparazi wetu hivi karibuni, Davina alisema kutokana na soko la filamu kuwa gumu wasanii wengi wameamua kugeukia biashara kwani wakikaa na kusubiria sanaa hiyo watakufa njaa.
“Tunapigana ili tulirudishe soko la filamu liwe kama zamani maana limekufa kutokana na filamu za mapenzi tunazocheza mara kwa mara. Kuna kila sababu ya kubadilika kama kweli tunataka kulishika soko,” alisema Davina.

Tupe Maoni Yako Kuhusu Habari Hii

 

GOSSIPS Copyright © 2016 -- Template created by Mbatta